Kocha wa timu ya taifa ya Ujeurmani Joachim Loew amesema kufufuka kwa timu ya taifa kumekuwa hatua nzuri sana, baada ya kuondolewa katika hali ya kukatisha tamaa na kwa fedhaha katika fainali za kombe la dunia mwaka 2018 nchini Urusi.
Katika mahojiano na gazeti la michezo la Kicker, Loew alikiri kwamba hakuona mapungufu yaliyopo yataathiri utendaji wa timu yake baada ya miezi 12 iliyopita kushuhudia awamu ya kufuzu iliyokuwa sahihi kabisa pamoja na iúbingwa wa kombe la shirikisho, Confederation.
Baada ya kombe la dunia alitarajia wachezaji kuamka katika ligi ya mataifa, lakini baada ya kipigo cha mabao 3-0 dhidi ya Uholanzi mwezi Oktoba alitanabahi kwamba “muda sasa umewadia wa mabadiliko”.