Makocha waendelea kuathiriwa na matokeo ya Afcon

133

Makocha  wawili  zaidi  wamepoteza  kazi  zao  na  mwingine  anatarajiwa  kibarua  kuota nyasi  katika  siku  za  hivi  karibuni  wakati  hali  hiyo  ikijitokeza katika  mashindano  ya  fainali  za  mataifa  ya  Afrika, AFCON, nchini  Misri  kwa  timu  ambazo  hazikutimiza  matarajio  ya  mashabiki  wake.

Paul Put  aliondolewa  na  Guinea  jana  Jumatatu  licha  ya  kukifikisha  kikosi  hicho  katika  awamu  ya  timu  16  bora  wakati Richardo Mannetti  mkataba  wake  haukurefushwa  baada  ya  Namibia  kupoteza  michezo  yake  yote  mitatu  ya  makundi.

Majaaliwa  ya  bingwa  mara  mbili  wa  taji  hilo  la  Afrika  Herve Renard   akiwa  na  kikosi  cha  Morocco  pia  inaonekana  kuelekea  mwisho  ambapo  vyombo  vya  habari  nchini  humo  jana  vilipigia  upatu  kuondoka  kwake  na  kocha  huyo kuweka  hali  yake  ya  baadaye  katika  hali  ya  kutojulikana  kwa  kutoa  taarifa  tata.

Kwa  ombi  langu, nimekutana  na  Fouzi Lekjaa, rais  wa  shirikisho  la  kandanda  la  Morocco, amesema  Renard.

Author: Bruce Amani